Académique Documents
Professionnel Documents
Culture Documents
1) Hali ya Uchaguzi
Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 kama
zilivyo chaguzi nyengine unakwenda sambamba na Uchaguzi Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Chaguzi hizo mbili zinafanyika
katika vituo sawa kwa kutumia utaratibu, ulinzi na usimamizi ulio sawa.
Kwa hivyo, siku ya uchaguzi mkuu mwananchi wa Zanzibar ndani ya
kituo kimoja anapiga kura tano (5) badala ya tatu (3) anazopiga
mwananchi aliyepo Tanzania Bara. Kura ambayo mwananchi wa
Zanzibar anapiga ni:
a)
b)
c)
d)
e)
Baada ya hapo Tume itajumlisha kura zote za Urais kutoka kila Jimbo.
Sheria ya Uchaguzi, kifungu cha 42(2) inaeleza kwamba Tume inaweza,
ikiwa itakuwa na sababu za msingi, kabla ya kutangaza matokeo kuagiza
kura katika majimbo au jimbo fulani kuhesabiwa upya.
Baada ya kujumuisha matokeo ya urais kutoka katika Majimbo, Sheria ya
Uchaguzi kifungu cha 42(3) kinaelekeza kwamba Tume itamtangaza
mshindi.
Tume ilifanya kazi ya kujumlisha matokeo ya Urais kutoka katika Majimbo
kama inavyoagizwa na Sheria. Baada ya majumuisho hayo, hakuna pahala
ambapo Tume iliagiza kura zihesabiwe upya kama Sheria inavyoagiza ikiwa
kutakuwa na sababu ya kufanya hivyo. Bila ya shaka kwa vile hakukuwa na
kasoro iliyopelekea haja ya kuhesabiwa upya Tume haikuchukua hatua hiyo.
Hadi kufikia tarehe 28 Oktoba, Tume ilishatangaza matokeo ya kura za
Urais kutoka katika majimbo 31; na ilishakamilisha kujumlisha matokeo ya
majimbo mengine 9 (ambayo ilikuwa bado haijayatangaza). Kwa maana
hiyo, kazi ya kujumlisha na kuhakiki matokeo ya majimbo 40 kati ya
majimbo 54 ilikuwa imeshakamilika. Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi
kifungu cha 42(6) Tume inatakiwa itangaze matokeo ndani ya siku 3 tokea
siku ya kupiga kura. Hivyo, tarehe 28 Oktoba ilikuwa ndiyo siku ya mwisho
ambayo Tume ilitakiwa itangaze matokeo ya Urais.
Hata hivyo, majumuisho ya matokeo ya Urais kupitia taarifa ambayo Tume
iliwapatia mawakala wa wagombea au wagombea wenyewe chini ya kifungu
cha 42(1) cha Sheria ya Uchaguzi baada ya kujumuishwa yalikuwa
yanaonyesha kwa ufupi kama ifuatavyo:
MGOMBEA KURA ZA
MGOMBEA
DR. ALI
182,011
MOHAME
D SHEIN
MAALIM
207,847
ASILIMIA
46.28%
52.84%
SEIF
SHARIF
HAMAD
IDADI YA
KURA HALALI
393, 323
ii.
10
11
12
13
14
15
Uchaguzi ipo juu ya Katiba na Sheria za nchi kwa vile Rais ana hiari
ya kusimamia vifungu vya Katiba vinavyosimamia nidhamu yao.
Kubwa zaidi kuliko yote ni kujiuliza iwapo mwendo huo wa Rais
hauendani kinyume na masharti ya kifungu cha 37(2) cha Katiba
kinachokataza Rais kufanya kitendo kinachokwenda kinyume na
Katiba na kwamba akifanya hivyo anaweza kushitakiwa mbele ya
Baraza la Wawakilishi.
Tafsiri sahihi ni kwamba Rais lazima ashike madaraka ya Urais na aachie
nafasi hiyo ndani ya muda huo wa miaka mitano isipokuwa kwa dharura
halali za kisheria ambazo zinakubalika. Ikiwa ukomo huo hautazingatiwa
basi Katiba yenyewe haitakuwa na maana na masharti yaliyowekwa
bayana tena kwa maandishi yatakuwa pia hayana maana. Aliyewahi
kuwa Jaji Mkuu wa Marekani, Justice John Marshall aliwahi kueleza haja
ya wanaotakiwa kulinda Katiba kutii masharti ya Katiba kwa kueleza
yafuatayo: to what purpose are powers limited, and to what purpose is
that limitation committed to writing, if these limits may, at any time, be
passed by those intended to be restrained? [Marbury v. Madison, pg 137]
Hivyo, mgogoro wa kwanza ni kutokuwepo Rais halali wa Zanzibar tokea
tarehe 3 Novemba, 2015. Pamoja na hali hiyo, anayedai kuendelea na
Urais amekuwa akifanya maamuzi makubwa yakiwemo ya uteuzi ambayo
yana athari kubwa hapo baadaye.
b) Kutokuwepo Mawaziri
Baraza la Wawakilishi tokea tarehe 12 Novemba, limemaliza muda wa
uhai wake kwa mujibu kifungu cha 92(1) cha Katiba. Hali hii ni tofauti
sana na kipindi ambacho Baraza limevunjwa chini ya vifungu vya 90(1)
na 91(1) vya Katiba. Katika Katiba ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya
Muungano na takriban katika nchi zote zenye asili ya mfumo wa
Westminster na hata mfumo wa Jamhuri (republican form of government)
zipo dhana mbili kuu kuhusiana na uhai wa Baraza la Wawakilishi
(Bunge). Dhana ya kwanza ni ya Baraza kuvunjwa (dissolution of
parliament) na dhana ya pili ni ile ya Baraza kumaliza muda wake (lapse
of tenure of Parliament). Dhana hizi mbili ni tofauti na zina athari tofauti
katika uhai wa Bunge na wa Serikali. Hata katika Katiba ya Zanzibar ya
16
17
18
MGOMBEA
DR. JOHN
POMBE
MAGUFULI
EDWARD
NGOYAYE
LOWASSA
KURA HALALI
194,317
ASILIMIA
46.5%
211,033
50.50%
IDADI YA KURA
HALALI
417,882
19
20
ii.
21
Kwa kuzingatia sababu zote hizo, ni wazi kuwa Hoja ya kurudiwa uchaguzi
haina uhalali, haina msingi na ni chachu ya kuiweka nchi katika utawala
usiokuwa halali na kusababisha fadhaa kubwa kwa wananchi. Ni hoja
ambayo inaweza kuzaa fujo na vurugu katika nchi na kupelekea mzozo
mkubwa zaidi wa kikatiba na kisheria. Sidhani kama tunataka tuifikishe
huko nchi na tuwafikishe huko wananchi tulioapa kuwatumikia na
kuwalinda.
22
23
Ukweli ni kwamba katika vikao hivyo vinane bado Dk. Ali Mohamed Shein
na Balozi Seif Ali Iddi wanangangania kurudia uchaguzi huku wakimtetea
kwa nguvu zote Jecha Salum Jecha, na mimi nimesisitiza haja ya kuheshimu
matakwa ya kikatiba na kisheria na maamuzi ya wananchi wa Zanzibar
waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015 katika uchaguzi ambao waangalizi
wote wa ndani na nje na hata Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar walisema kwamba ulikuwa huru, wa haki na uliofanyika katika hali
ya amani.
Kwa hakika hadi jana, ukiangalia tovuti ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
utaona taarifa zinazosema kwamba uchaguzi hadi hatua ya kuhesabu kura
ulifanyika kwa utulivu nchi nzima.
Kutokana na kutofikia muafaka pamoja, tulikubaliana kuandaa taarifa ya
pamoja ambayo ilielezwa kwamba ingeandaliwa na Katibu wa vikao hivyo
lakini sasa ni zaidi ya wiki mbili, hakuna kikao kilichoitishwa. Nimeandika
barua kuhimiza kikao cha kupokea taarifa hiyo na kuipitisha lakini bado Dk.
Shein anasema wanahitaji muda.
Ni wazi kwamba Dk. Ali Mohamed Shein hakuwa na nia njema katika
mazungumzo haya na amepoteza sifa ya kuongoza vikao hivyo.
6. NJAMA ZA CHINI KWA CHINI ZA KUHUJUMU UTAFUTAJI
WA UFUMBUZI WA HAKI
Wakati Dk. Ali Mohamed Shein akikwepa kwa makusudi kuitisha kikao cha
kupokea taarifa ya mazungumzo hayo, tumegundua kwamba lengo halisi ni
kuisindikiza Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kutangaza tarehe ya uchaguzi
wa marudio ili baadaye itolewe hoja kwamba suala hilo limeshaamuliwa.
Tunazo taarifa za uhakika kwamba Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
imetakiwa kukutana tarehe 14 Januari, 2016 kwa lengo la kutangaza tarehe
ya uchaguzi wa marudio ambao unatajwa kuwa umepangwa ufanyike tarehe
28 Februari, 2016.
Taarifa hizo zinaeleza kwamba lengo la hatua hiyo ni kukwamisha juhudi
zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa
24
25
26
HITIMISHO
Zanzibar imepita katika siasa za dhoruba na machafuko kwa zaidi ya miaka 50.
Dhoruba na machafuko hayo yalifikia hadi kugharimu maisha ya watu. Ni kwa
sababu ya kuchoshwa na siasa za aina hiyo na migogoro isiyokwisha ndiyo
maana mwaka 2009, mimi na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Amani Karume,
tulichukua maamuzi ya kijasiri ya kuleta MARIDHIANO ambayo yaliituliza
Zanzibar. Kila mmoja wetu ni shahidi kwamba kwa miaka sita iliyopita Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ilipumua kujibu hoja zisizokwisha kuhusu hali ya
kisiasa Zanzibar na badala yake tukawa tunapongezwa kwa kuleta maridhiano
na kuanzisha muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Hatukutegemea
kwamba baada ya kazi ile kubwa, sasa kutazuka kikundi cha viongozi
waliopewa dhamana ya kuwaunganisha watu wafanye kazi ya kuyabomoa
Maridhiano yetu na kuturudisha kwa nguvu kule tulikotoka. Watu hawa
hawapaswi kupewa nafasi kufanikisha dhamira yao hiyo ovu. Na Wazanzibari
hawatowapa nafasi hiyo. Ni kwa sababu hiyo tumeamua kuzungumza na
Watanzania na kuwajuvya haya ili kuzuia nchi yetu isivurugwe na kurudishwa
tulikotoka.
27