Académique Documents
Professionnel Documents
Culture Documents
Ifuatayo ni taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha Januari hadi
Disemba, 2017. Taarifa hii inaonesha matukio makubwa na madogo ya uhalifu, matukio
ya usalama barabarani, matukio yaliyovuta hisia kwa jamii, hali ya ulinzi na usalama
kipindi cha sikukuu ya Kristmasi na mwaka mpya 2018, mpango mkakati wa Jeshi la
Polisi Mbeya na mafanikio yaliyopatikana kutokana na operesheni, misako na doria.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye
tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa
likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na
uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa
matukio makubwa ya uhalifu kwa mwaka huu 2017.
Jumla ya makosa ya jinai 26,009 yaliripotiwa kutokea mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha
mwaka 2017 ikilinganishwa na matukio 32,943 yaliyoripotiwa kipindi kama hicho
Mwaka 2016. [-21].
Ajali za majeruhi mwaka 2017 zilikuwa 103 wakati mwaka 2016 zilikuwa 211.[-51]
Watu waliojeruhiwa mwaka 2017 walikuwa 268 wakati mwaka 2016 walikuwa 482.
[-44]
Aidha baadhi ya sababu za kutokea kwa matukio ya ajali ni kuongezeka kwa vyombo
vya usafiri mkoani Mbeya hasa magari na pikipiki, baadhi ya madereva kutozingatia
sheria za usalama ikiwa ni pamoja na mwendo kasi hasa usiku na ulevi licha ya jitihada
za Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na baadhi ya wadau kutoa elimu
hiyo mara kwa mara. Hali ya hewa hususani ukungu na utelezi katika baadhi ya
maeneo ya barabara ya Mbeya / Rungwe / Kyela.
Bhangi uzito wa kilo 403 na gram 394 ilikamatwa ikiwa ni pamoja na mashamba
makubwa 6 tofauti yenye ukubwa wa ekari 13 ½ ilivunwa na kuharibiwa kwa
kuchomwa moto.
Mirungi kilo 4 pamoja na shamba moja lenye ukubwa wa nusu ekari ilivunwa na
kuharibiwa kwa kuchomwa moto.
Dawa za kulevya aina ya heroine gram 196 ilikamatwa
Dawa ya kulevya aina ya amphetermine gram 20 ilikamatwa.
Bidhaa za magendo zenye thamani ya Tshs 81,930,000/= ikiwemo bidhaa za
magendo vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku na serikali vyenye
viambata vya sumu, pombe kali na mahindi tani 60 na magunia 223 yaliyokuwa
yakiingizwa nchini kutoka malawi yalikamatwa.
Nyara za Serikali zenye thamani Tshs 379,604,000/= na USD 300 zilikamatwa.
Wahamiaji haramu 344 walikamatwa wakiwemo Ethiopia 240, Malawi 48,
Somalia 37, Burundi 17, Botswana 1 na Zambia 1. Pia magari 3 yalikamatwa
yakisafirisha wahamiaji haramu hao ambayo ni T. 347 DAJ toyota haice, T. 917
AWM aina ya fuso na T.155 AZU aina ya isuzu canter pamoja na wasafirishaji 7
watanzania wamefikishwa mahakamani pamoja na magari hayo
Pombe haramu ya moshi gongo ujazo wa lita 3,719 pamoja na mitambo 33
ilikamatwa.
Jumla ya silaha 28 zilikamatwa ikiwemo shortgun 17, risasi 202, Riffle 2 na risasi
47, gobole 8 na bastola 1.
Sare za JWTZ “kombati” suruali 2, mashati 2, kofia 2 na viatu / mabuti jozi
mbili zilikamatwa.
Pombe kali zilizopigwa marufuku na serikali zenye vifungashio vya plastiki
zenye thamani ya zaidi ya Tshs 1,023,508, 750/= zilikamatwa maeneo mbalimbali
mkoani Mbeya na kuzuiliwa kusubiri maelekezo toka serikalini.
Noti bandia Tshs 1,245,000/= na USD 1,199 zilikamatwa.
Tozo [Notification] Tshs 2,380,050,000/= zilipatikana.
WITO WA KAMANDA:
Pia natoa shukrani zangu za dhati kwa waandishi wa habari na vyombo vyote vya habari
kwa ushirikiano wetu kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya katika kipindi cha mwaka
2017, kwa nafasi hii ninaomba ushirikiano huu uendelee katika kipindi cha mwaka 2018.
Aidha anatoa wito kwa wazazi/walezi kuzingatia utoaji wa malezi bora kwa
watoto/vijana ili wakue katika misingi mizuri ya maadili mema katika jamii na
kujiepusha na matukio ya kihalifu na kukataa uhalifu wangali wadogo ikiwa ni pamoja
na kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya, kucheza kamari na ulevi uliopitiliza.
Kwa kutambua kuwa suala la ulinzi na usalama unaanzia ngazi ya familia, mtaa,
kitongoji, kijiji, kata, tarafa, wilaya hadi ngazi ya mkoa, ni vema kila mmoja wetu
kutambua na kuamini usalama wa mali na maisha yetu unaanzia na mimi, wewe na sisi
sote. Kwa kuimarisha ulinzi na usalama wetu na mali zetu inatoa fursa kwa wawekezaji
kuwekeza katika mkoa wetu, wananchi kujiajiri na kuajiriwa ikiwa ni pamoja na
kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii bila kuathiri amani na
utulivu.
Aidha Kamanda MPINGA anatoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na
wahalifu, kushirikiana na vikundi vya ulinzi shirikishi vilivyopo katika maeneo yao.
Pia kwa watumiaji wa vyombo vya moto kuheshimu sheria na alama za usalama
barabarani, watembea kwa miguu kuzingatia alama za barabarani ili kuepuka ajali
zinazoweza kuepukika.
Imesainiwa na:
[MOHAMMED R. MPINGA - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.