Vous êtes sur la page 1sur 5

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


JESHI LA POLISI TANZANIA

Ofisi ya Kamanda wa Polisi,


Mkoa wa Mbeya,
Namba ya simu 2502572 S. L. P. 260,
Fax - +255252503734 MBEYA.
E-mail:- rpc.mbeya@tpf.go.tz
tanpol.mbeya@gmail.com

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI


“PRESS RELEASE” TAREHE 04.01.2018.

Ifuatayo ni taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha Januari hadi
Disemba, 2017. Taarifa hii inaonesha matukio makubwa na madogo ya uhalifu, matukio
ya usalama barabarani, matukio yaliyovuta hisia kwa jamii, hali ya ulinzi na usalama
kipindi cha sikukuu ya Kristmasi na mwaka mpya 2018, mpango mkakati wa Jeshi la
Polisi Mbeya na mafanikio yaliyopatikana kutokana na operesheni, misako na doria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye
tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa
likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na
uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa
matukio makubwa ya uhalifu kwa mwaka huu 2017.

1. MATUKIO MAKUBWA NA MADOGO YA JINAI.

Jumla ya makosa ya jinai 26,009 yaliripotiwa kutokea mkoa wa Mbeya kwa kipindi cha
mwaka 2017 ikilinganishwa na matukio 32,943 yaliyoripotiwa kipindi kama hicho
Mwaka 2016. [-21].

Makosa makubwa yaliyoripotiwa mwaka 2017 yalikuwa ni 2,234 ikilinganishwa na


matukio 2,071 yaliyoripotiwa mwaka 2016. [+8] Makosa madogo 23,775 yaliripotiwa
mwaka 2017, ikilinganishwa na makosa 30,872 yaliyoripotiwa mwaka 2016. [-23].
Aidha jumla ya makosa 734 yaliripotiwa mwaka 2017 kutokana na jitihada za Jeshi la
Polisi kwa kushirikiana na wananchi na wadau wengine kupitia misako, doria na
operesheni mbalimbali ikilinganishwa na matukio 565 yaliyoripotiwa mwaka 2016.
[+30].

2. MATUKIO YA USALAMA BARABARANI.


Kwa upande wa makosa ya usalama barabarani jumla ya makosa yote ya ajali pamoja
na ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani kwa kipindi cha mwaka 2017 yalikuwa
82,211 wakati kipindi kama hicho mwaka 2016 yalikuwa 66,172. [+24]
Matukio ya ajali kwa mwaka 2017 yalikuwa 244 ikilinganishwa na matukio 393
yaliyoripotiwa mwaka 2016.[-38]. Ajali zilizosababisha vifo mwaka 2017 zilikuwa
141, wakati mwaka 2016 zilikuwa 182.[-22.5]. Watu waliokufa mwaka 2017
walikuwa 170, wakati mwaka 2016 walikuwa 286. [- 40.5].

Ajali za majeruhi mwaka 2017 zilikuwa 103 wakati mwaka 2016 zilikuwa 211.[-51]
Watu waliojeruhiwa mwaka 2017 walikuwa 268 wakati mwaka 2016 walikuwa 482.
[-44]

Pesa zilizokusanywa kutokana na makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa sheria za


usalama barabarani [notification] mwaka 2017 zilikuwa Tshs 2,380,050,000/=, wakati
kipindi cha mwaka 2016 zilikusanywa Tshs 1,920,900,000/= [+24]

Aidha baadhi ya sababu za kutokea kwa matukio ya ajali ni kuongezeka kwa vyombo
vya usafiri mkoani Mbeya hasa magari na pikipiki, baadhi ya madereva kutozingatia
sheria za usalama ikiwa ni pamoja na mwendo kasi hasa usiku na ulevi licha ya jitihada
za Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na baadhi ya wadau kutoa elimu
hiyo mara kwa mara. Hali ya hewa hususani ukungu na utelezi katika baadhi ya
maeneo ya barabara ya Mbeya / Rungwe / Kyela.

3. MATUKIO YALIYOVUTA HISIA KWA JAMII.


Jumla ya matukio matatu makubwa yaliyovuta hisia kwa kamii yaliripotiwa kama
ifuatavyo : -
i. JALADA LA UCHUNGUZI:
Tarehe 16.01.2017 saa 12:30hrs mtaa wa Igoma [A] kata Isanga, tarafa Sisimba
jiji na mkoa wa Mbeya kulitokea tukio la waombolezaji kuzika jeneza tupu na
mwili wa marehemu mtoto HARUN JAILO KYANDO [9] Mkazi wa mtaa wa
Igoma [A] kusahaulika nyumbani. Hata hivyo mwili huo baadae ulizikwa upya
kwa kufuata taratibu.

ii. JALADA LA UCHUNGUZI:


Tarehe 15.02.2017 BARAKA S/O MWAFUNGO, miaka 22, msafwa, mkulima,
mkazi wa Pipeline alifariki dunia kwa maradhi ya kisukari. Tarehe 18.02.2017
RUTH SEGETI [57] Mkazi wa Pipeline mama mzazi wa marehemu akiwa na
vijana wawili walifukua kaburi la mtoto wake na kutoa mwili huo kisha kuupeleka
nyumbani kwake na kuuhifadhi kwa imani kuwa atafufuka. Hata hivyo mwili wa
marehemu baadae ulizikwa upya tarehe 20.02.2017 kwa usimamizi wa
Halmashauri ya wilaya Mbeya Vijijini.

iii. AJALI YA MOTO KUSABABISHA UHARIBIFU.


Tarehe 15.08.2017 saa 21:30hrs eneo la SIDO Mwanjelwa katika soko la Sido,
lililopo Sido, kata ya Iyela, tarafa Iyunga jiji na mkoa wa Mbeya kulitokea ajali ya
moto ambapo baadhi ya maduka / vibanda vya soko hilo liliteketea kwa moto.
Hakuna madhara kwa binadamu. Thamani ya mali iliyoteketea inakadiliwa ni
zaidi ya Tshs 500,000, 000/=.
4. HALI YA ULINZI NA USALAMA KIPINDI CHA SIKUKUU ZA KRISMAS
NA MWAKA MPYA – 2018.
Katika kipindi cha sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya 2018 kwa ujumla hali ilikuwa
ni shwari, ulinzi uliimarishwa maeneo mbalimbali ikiwemo nyumba za ibada, kumbi za
starehe, barabara kuu na maeneo yenye mikusanyiko ya watu.
Hata hivyo kuna matukio kadhaa ya uvunjifu wa amani yaliripotiwa kutokea kama
kawaida kama ifuatavyo:-
- Mauaji - 1
- Kujeruhi - 1
- Ajali ya kifo – 1

Upande wa misako ni kama ifuatavyo:-


- Bhangi gram 35
- Pombe haramu ya moshi [gongo] lita 124
- Silaha 3 aina tofauti Riffle 1, Shortgun 1 na Gobole 1 pamoja na risasi 8 za
Shortgun na 2 za Riffle.
- Wahamiaji haramu 17 wote raia wa Ethiopia
- Risasi 81 za aina ya Riffle / Marv IV ziliokotwa na Polisi
- Gari 2 aina ya Fuso zenye namba T. 394 BCL na T. 399 DCC na watuhumiwa 5
wakisafirisha milipuko bila kibali aina ya Magzan – Kubella tani 20 kutoka [W]
Chunya kuelekea mkoa wa Geita.
- Upande wa Usalama barabarani tozo Tshs 47,160,000/= zilipatikana.

5. MKAKATI NA MPANGO KAZI WA KUZUIA UHALIFU


Miongoni mwa mikakati/mpango kazi wa kuzuia uhalifu Mkoani Mbeya ni pamoja na :-

 Kufanya tathmini ili kuyatambua matishio katika maeneo yetu na mikakati ya


kupunguza uhalifu ulioongezeka zaidi mwaka 2017.
 Kubaini muelekeo wa uhalifu na maeneo tete uhalifu ili kuelekeza nguvu za ziada
katika maeneo hayo [Crime threat analysis].
 Kuchukua hatua za haraka pale tukio linapotokea na kulitolea taarifa.
 Kuendelea na jitihada za kushawishi Halmashauri za Jiji/Miji/Wilaya katika
kupambana na uhalifu. Hata hivyo changamoto iliyopo ni kwa Halmashauri hizo
kutotambua kuwa jukumu la kuihakikishia jamii usalama wa maisha, mali, amani
na utulivu ni moja ya majukumu yake ya msingi kwa mujibu wa sheria namba 7
ya mwaka 1982 ya sheria za Serikali za Mitaa [Serikali za Wilaya] pamoja na
sheria namba 8 ya mwaka 1982 , sheria ya Serikali za Mitaa [Mamlaka za Miji].
 Kuongeza jitihada kwenye doria na misako yenye tija na ufanisi
 Kuongeza kasi ya kueneza falsafa ya ulinzi shirikishi
 Kuendelea kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ikiwa ni
pamoja na taasisi za Serikali na vyombo vya udhibiti kama vile JWTZ,
JKT,Magereza, Uhamiaji,Usalama wa Taifa, Zima Moto na Uokoaji Takukuru,
Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali, TRA, TFDA n.k.
 Kudumisha ushirikiano na vyombo vya habari vilivyopo Mkoa wa Mbeya.
 Ushirikiano na Mikoa jirani [INTER-REGION CO-OPERATION] katika
kupeana taarifa za uhalifu na wahalifu.
 Ushirikiano na madhehebu ya dini, wazee wa mila, viongozi wa Serikali za Mitaa,
Kata, Tarafa na viongozi wa Vyama vya Siasa katika kupambana na uhalifu na
wahalifu.
 Kuimarisha utendaji wa weledi
 Kujenga na kuimarisha uaminifu na uadilifu wa askari wetu.
 Kuimarisha utoaji huduma bora kwa wananchi [Customer Care].

6. MAFANIKIO YALIYOPATIKANA KUTOKANA NA MISAKO, DORIA NA


OPERESHENI.
Baadhi ya mafanikio yaliyopatikana kutokana na jitihada za Jeshi la Polisi kwa
kushirikiana na wananchi na wadau wengine ni :-

 Bhangi uzito wa kilo 403 na gram 394 ilikamatwa ikiwa ni pamoja na mashamba
makubwa 6 tofauti yenye ukubwa wa ekari 13 ½ ilivunwa na kuharibiwa kwa
kuchomwa moto.
 Mirungi kilo 4 pamoja na shamba moja lenye ukubwa wa nusu ekari ilivunwa na
kuharibiwa kwa kuchomwa moto.
 Dawa za kulevya aina ya heroine gram 196 ilikamatwa
 Dawa ya kulevya aina ya amphetermine gram 20 ilikamatwa.
 Bidhaa za magendo zenye thamani ya Tshs 81,930,000/= ikiwemo bidhaa za
magendo vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku na serikali vyenye
viambata vya sumu, pombe kali na mahindi tani 60 na magunia 223 yaliyokuwa
yakiingizwa nchini kutoka malawi yalikamatwa.
 Nyara za Serikali zenye thamani Tshs 379,604,000/= na USD 300 zilikamatwa.
 Wahamiaji haramu 344 walikamatwa wakiwemo Ethiopia 240, Malawi 48,
Somalia 37, Burundi 17, Botswana 1 na Zambia 1. Pia magari 3 yalikamatwa
yakisafirisha wahamiaji haramu hao ambayo ni T. 347 DAJ toyota haice, T. 917
AWM aina ya fuso na T.155 AZU aina ya isuzu canter pamoja na wasafirishaji 7
watanzania wamefikishwa mahakamani pamoja na magari hayo
 Pombe haramu ya moshi gongo ujazo wa lita 3,719 pamoja na mitambo 33
ilikamatwa.
 Jumla ya silaha 28 zilikamatwa ikiwemo shortgun 17, risasi 202, Riffle 2 na risasi
47, gobole 8 na bastola 1.
 Sare za JWTZ “kombati” suruali 2, mashati 2, kofia 2 na viatu / mabuti jozi
mbili zilikamatwa.
 Pombe kali zilizopigwa marufuku na serikali zenye vifungashio vya plastiki
zenye thamani ya zaidi ya Tshs 1,023,508, 750/= zilikamatwa maeneo mbalimbali
mkoani Mbeya na kuzuiliwa kusubiri maelekezo toka serikalini.
 Noti bandia Tshs 1,245,000/= na USD 1,199 zilikamatwa.
 Tozo [Notification] Tshs 2,380,050,000/= zilipatikana.
WITO WA KAMANDA:

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi MOHAMMED R.


MPINGA anatoa pongezi kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kwa ushirikiano wao
wa dhati kwa Jeshi la Polisi katika mapambano dhidi ya uhalifu na wahalifu kupitia
dhana ya ulinzi shirikishi na Polisi jamii katika kipindi chote cha Januari hadi
Desemba – 2017, aidha anatoa rai kwa jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi
katika kipindi chote ili kuhakikisha mkoa wetu wa Mbeya unakuwa salama.

Pia natoa shukrani zangu za dhati kwa waandishi wa habari na vyombo vyote vya habari
kwa ushirikiano wetu kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya katika kipindi cha mwaka
2017, kwa nafasi hii ninaomba ushirikiano huu uendelee katika kipindi cha mwaka 2018.

Aidha anatoa wito kwa wazazi/walezi kuzingatia utoaji wa malezi bora kwa
watoto/vijana ili wakue katika misingi mizuri ya maadili mema katika jamii na
kujiepusha na matukio ya kihalifu na kukataa uhalifu wangali wadogo ikiwa ni pamoja
na kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya, kucheza kamari na ulevi uliopitiliza.

Kwa kutambua kuwa suala la ulinzi na usalama unaanzia ngazi ya familia, mtaa,
kitongoji, kijiji, kata, tarafa, wilaya hadi ngazi ya mkoa, ni vema kila mmoja wetu
kutambua na kuamini usalama wa mali na maisha yetu unaanzia na mimi, wewe na sisi
sote. Kwa kuimarisha ulinzi na usalama wetu na mali zetu inatoa fursa kwa wawekezaji
kuwekeza katika mkoa wetu, wananchi kujiajiri na kuajiriwa ikiwa ni pamoja na
kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii bila kuathiri amani na
utulivu.

Aidha Kamanda MPINGA anatoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na
wahalifu, kushirikiana na vikundi vya ulinzi shirikishi vilivyopo katika maeneo yao.
Pia kwa watumiaji wa vyombo vya moto kuheshimu sheria na alama za usalama
barabarani, watembea kwa miguu kuzingatia alama za barabarani ili kuepuka ajali
zinazoweza kuepukika.

Imesainiwa na:
[MOHAMMED R. MPINGA - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Vous aimerez peut-être aussi