Académique Documents
Professionnel Documents
Culture Documents
UTANGULIZI
Sekta ya uziduaji (madini, mafuta na gesi asilia) ni kichocheo kwa ukuaji wa uchumi wa
nchi. Kwa ukubwa wake, sekta hii inakadiriwa kuwa na thamani ya shilingi za Kitanzania
milioni 4,975,991. Na huchangia asilimia 4.8 ya Pato la Taifa. Kwa sababu hii, sisi
HakiRasilimali-PWYP, jukwaa la Asasi za Kiraia linalochambua sera na kufanya
uchechemuzi katika sekta hii nchini Tanzania, tumefuatilia kwa umakini mwelekeo wa
kisera na majadiliano na maoni mbalimbali kwa shauku kubwa katika kipindi cha mwaka
mmoja uliopita.
Kwa minajili hiyo, tumejadili na kuchambua mwelekeo wa kisera katika sekta hii kwa lengo
la kutoa maoni yetu ili kuainisha maeneo yanayohitaji kupewa kipaumbele kwenye Bajeti
ya Wizara ya Madini kwa Mwaka 2018/19. Lengo kuu ni kuboresha usimamizi na
kuhakikisha kwamba mapato yanayopatika katika sekta hii yanaleta tija itakayochangia
kwenye kunufaisha Watanzania kwa ujumla.
MWELEKEO WA KISERA
Hata hivyo TEITI imekua ikitengewa pesa kidogo sana kutoka serikalini na kutegemea
ufadhili mkubwa kutoka kwa wahisani kutoka nje ya nchi kitu ambacho kinafanya kazi za
taasisi hii kususua na kukosa uhakika haswa wakati huu ambao michango ya wafadhili
kutoka nje imekwisha.
Uchumi wa nchi unaonekana kukuwa kwa wastani wa 6.8% Katika kipindi cha robo tatu
za mwanzo za mwaka wa fedha 2017/2018, na shughuli za madini zikionekana kukuwa
kwa kasi zaidi kwa 24.3% ukiliganisha na sekta nyingine. Kutokana na ukuwaji huo wa
kasi na mwenendo wa kibajeti hususani kwa makusanyo yanayofanywa na wizara husika
kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita, inatoa muelekeo wa ongezeko la ukusanywaji wa
mapato katika sekta na wizara husika kwa mwaka 2017/2018. Kati ya mwaka wa fedha
2015/2016 iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini ilikusanya asilimia 75 ya makadirio yake
na kwa mwaka 2016/2017 makusanyo yalikuwa asilimia 72 ya makadirio yake. Lakini pia,
tumeona punguzo la asilimia katika changio kutoka kwenye sekta ya uziduaji kwenda
kwenye bajeti ya taifa mwaka wa fedha 2017/18.
Waziri Mkuu wakati akiwasilisha bungeni hotuba kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za
Serikali kwa Mwaka 2017/2018 alisisitiza kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha
2017/2018 maduhuli ya Serikali yaliyokusanywa kutoka katika sekta ya madini yalifikia
shilingi bilioni 180.4. Pia Serikali iliendesha zoezi la ukaguzi na kuwezesha kukamatwa kwa
madini yaliyokuwa yakitoroshwa yenye jumla ya thamani ya Dola za Marekani takriban
898,523 na shilingi milioni 557 ambayo yalifanyiwa mnada hapahapa nchini.
Lakini pia, mwaka huo huo, Serikali kupitia wizara ya Nishati na Madini, ilikuwa na
vipaumbele mbalimbali vilivyolenga kuhakikisha nchi inapata mapato sahihi yatokanayo
na madini. Katika kuhakikisha hilo, Aprili 2018, Serikali ilizindua ukuta uliozunguka
machimbo ya Tanzanite kwa lengo la kuimarisha udhibiti wa utoroshwaji wa madini na
kuhakikisha Serikali haipotezi mapato kutokana na utoroshwaji wa madini aina ya
Tanzanite kwa njia zisizo halali. Mbali na hilo pia kulifanyika mnada mkubwa wa
Tanzanite yenye uzito wa gramu 47,201 iliyouzwa kwa shilingi 1,839,476,075 (Serikali
ilipata mrabaha wa shilingi millioni 110.3 kama ada ya ukaguzi). Makusanyo mengine mbali
na bajeti iliyopangwa na Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18 yalitokana na
mazungumzo yaliyofanywa kwa niamba ya umma kati ya serikali na kampuni ya Acacia,
iliyotoa kiasi cha dola za Kimarekani milioni 330 kwa lengo la kukomesha mgogoro
ambao ungepinga shughuli zake nchini.
Aidha, Mwenyekiti Mtendaji wa Barrick Gold John Thornton, alisema kampuni hiyo ya
madini itatoa kwa Tanzania hisa za asilimia 16 katika migodi yake mitatu (3) na asilimia
50 katika makusanyo ya mapato katika migodi hiyo.
Tegemeo letu ni kuona ongezeko la bajeti kwa mwaka wa fedha 2018/19. Lakini pia kupata
ufafanuzi kwa namna gani makusanyo yaliyofanyika nje ya bajeti iliyopitishwa mwaka
2017/18 yametumika katika miradi ya maendeleo nchini
CHANGAMOTO: